• Kuhudhuria Mkutano Mkuu na Mikutano mingine itakayoitishwa na TASSIM. 
  • Kuomba na kupata taarifa muhimu kutoka TASSIM.
  • Kupata majarida na habari zinginezo zinazotolewa na TASSIM. 
  • Upatikanaji wa rasilimali muhimu ambazo zitatolewa na TASSIM. 
  • Haki ya kupiga na kupigiwa kura. 
  • Haki ya kupewa kipaumbele cha kuwa mshauri kwenye mikataba ya TASSIM kulingana na vigezo na masharti ya TASSIM. 
  • Kupewa kipaumbele cha kushiriki kwenye mikutano na majukwaa ya kimkakati yaliyoandaliwa na taasisi zingine kama mwakilishi kutoka TASSIM. 
  • Kupata kipaumbele cha kushiriki kwenye kamati za ufundi. 
  • Kupata punguzo la asilimia 20% kwenye ada ya usajili wa kozi, semina, mikutano na majukwaa yanayoandaliwa na TASSIM.